Njia rahisi ya kunyoa ndevu bila kusababisha upele

Njia rahisi ya kunyoa ndevu bila kusababisha upele

Kwa wastani binadamu anatumia miezi (5) mitano ya maisha yake kushave na ndani ya miezi hiyo mitano kwa mwanaume atashave mara elfu 20,000 katika muda wa maisha yake yote.Baadhi ya watu huchukia kabisa ikifika kipindi cha kushave kutokana na changamoto wanazozipata wakati na baada ya kushave.

Kushave kuna changamoto nyingi,  haijalishi ni unashave ndevu (mwanaume), sehemu za kwapa au sehemu nyeti.Changamoto hizo zinaweza kua:

  1. Kupata vipele baada ya kunyoa hasa kwenye maeneo yanayozunguka kidevu,  kwapani na weusi.2. Ngozi kuwasha, kutokana na ukavu unaosababishwa na spirit au bidhaa yenye alcohol inayopakwa kweny ngozi.3. Kupata weusi baada ya michubuko na vipele baada ya kunyoa kupona vinaacha weusi sehemu husika.

Changamoto hizi zinachangiwa zaidi na bidhaa na vifaa tunavyotumia kunyolea. Sio wote wanapata vipele na weusi,  ila kwa wale wenye vipele na weusi kwenye maeneo wanayoshave, hiyo inachangiwa na vitu vifuatavyo:1.kushave bila kulainisha ngozi2.Kupaka spirit au aftershave yenye alcohol baada ya kushave3.kutokupaka kitu chochote baada ya kushave4.kutumia blade ama kiwembe kisicho na makali.Utumie nini ili usipate vipele na uondoe weusi?1. Lainisha Ngozi kabla ya kunyoaNi muhimu kulainisha ngozi yako kabla ya kunyoa kwa, layer ya juu ya ngozi ina chembe hai zilizokufa,  ukilainisha ngozi kabla ya kunyoa itasaidia kuondoa na chembe hai zilizokufa wakati wa kunyoa,  pia itasaidia wembe kuteleza vizuri kwenye ngozi bila kusababisha michubuko.

Aloe liquid soap ni nzuri kwa kunyolea,  ina ph sawa na ngozi yako hivyo haiui bacteria wazuri waliopo kwenye ngozi, ina aloe vera itakayoipa ngozi yako unyevu nyevu unaohitajika wakati wa kunyoa.2.Tumia aftershave baada ya kunyoa.unatakiwa kutumia aftershave ili kupoza ngozi,  kuipa unyevu nyevu na kufanya nyororo.  Spirit na aftershave zenye alcohol zinafanya ngozi kuwa kavu, itasababisha miwasho na ukijikuna ndo inapelekea kutoka vipele.

Gentlemans pride aftershave ina stabilized aloe vera itakayopoza na kuponya ngozi na michubuko iliyosababishwa na kiwembe,  haina alcohol hivyo haichomi,  itaipa ngozi unyevu nyevu na unyororo ili kuzuia miwasho.3. Nyoa kufatisha muelekeo wa nywele zilivyoota. Hii itasaidia ngozi isiume zaidi wakati wa kunyoa.  Pia hakikisha kiwembe au blade unayotumia kunyolea ni kikali, kikiwa butu Utarudi mara nyingi na kuumiza zaidi ngozi.4. Usitumie deodorant yenye chumvi ya aluminum na alcohol.Chumvi ya aluminum na alcohol inachangia kufanya ngozi iwe kavu na kuwasha baada ya kunyoa ambayo itapelekea kupata weusi wa kwapa.

Aloe vera shield deodorant haina chumvi ya aluminum na unaeza kuitumia hata baada ya kushave na inasaidia kuondoa weusi wa kwapa.

Haiyaa haiyaa ndugu zangu wa scoop natumai hizo tips zitasaidia vijana wengi na wazee wengi kuondokana na tatizo la kutoka vipele wakishamaliza kushave, usisahau kudondosha comment yako hapo chini kutujuza ni kitu gani unatamani kujifunza mdau wetuu.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post