Nick Cannon asahau jina la mtoto wake wa 12

Nick Cannon asahau jina la mtoto wake wa 12

Rapa na mtangazaji Nick Cannon moja ya mastar wenye watoto wengi zaidi na mama tofauti, Cannon ambae ana watoto 12 wa mama tofauti kupitia moja ya mahojiano yake alisahau jina la mwanae wa mwisho wa 12 jambo amabalo limewaacha hoi mashabiki zake.

Katika mahojiano hayo Nick alisema anaweza kutaja majina ya watoto wake wote ila alisahau jina la mtoto wake wa mwisho Onyx, ambapo baadhi ya watu na mashabiki zake wameshangazwa na tukio hilo huku wakitaka Cannon apumzike kwenye swala la kuongeza mtoto mwingine wa 13.

Ikumbukwe tuu siku za hivi karibuni rapa huyo alieleza kuwa anatamani kuongeza mtoto mwingine wa 13 na akamchagua kabisa mtu anae tamani kuzaa nae ambae ni Taylor.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post