Mwanamke wa miaka 70 ajifungua mapacha

Mwanamke wa miaka 70 ajifungua mapacha

Mwanamke mmoja kutoka nchini #Uganda aitwaye, Safina Namukwaya mwenye umri wa miaka 70 amezua gumzo mitandaoni baada ya kujifungua watoto mapacha akiwa na umri huo.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo vimeeleza kuwa #Safina amejifungua mapacha wawili, mmoja akiwa wa kiume na mwingine wakike katika kituo cha upandikizaji cha Women’s Hospital Internation and Fertility Center kilichopo nchini humo.

Aidha kwa mujibu wa ripoti imeelezwa kuwa mwanamke huyo amepata ujauzito kwa njia ya kupandikizwa, licha ya hayo pia alipata wasaha wa kuzungumza na #NTVnews na kueleza kuwa hii si mara ya kwanza kupata mtoto kwa njia hiyo, mwaka 2020 alifanikiwa kupata mtoto wa kike aitwaye #Sarah.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post