Mo Salah aomba viongozi kuingilia vita ya Palestina na Israel

Mo Salah aomba viongozi kuingilia vita ya Palestina na Israel

Mchezaji wa ‘klabu’ ya #LiverPool #MoSalah ametoa wito kwa viongozi wote duniani akiwataka kukutana pamoja kutoa msaada wa haraka wakati wa mzozo kati ya Israel na Palestina.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram na X ‘ameposti’ video yake akieleza jinsi gani anavyo guswa na vita hiyo na kuwataka viongozi wote duniani wakutane ili waweze kutoa msaada wa haraka ili kutatua vita hiyo ambayo inazidi kupoteza watu kwa vifo hasa watoto na wanawake.

 Mo Salah ameonesha hali ya kuhuzunishwa na ghasia hiyo inayo endelea kati ya mataifa hayo mawili ikiwa mpaka sasa hakuna njia iliyopatikana kutuliza vurugu hizo zinazoendelea.
.
.
.
#MwanachiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post