MAUJANJA YA VPN

MAUJANJA YA VPN

Wengi wameijua zaidi baada ya kushindwa kutumia mitandao yao ya kijamii mwaka jana mwishoni, lakini VPN ni teknolojia ambayo imekuwepo kwa muda mrefu sana, na hutumika zaidi katika nchi zenye vizuizi katika utumiaji wa kimtandao, kama vile nchi ya China.

Huku kukiwa kuna tafrani za hapa na pale kuhusu hii teknolojia, leo tunakuangazia kuhusu VPN, inavyofanya kazi, Pamoja na faida na hasara zake.

VPN NI NINI?

Neno VPN ni kifupi cha maneno “VIRTUAL PRIVATE NETWORK”, ikimaanisha mtandao binafsi, ambao unatumia mfumo fulani ulioitwa “tunnel” ama ‘handaki’, unoaruhusu shughuli zako za mtandao zionekane kwa watu wasiohusika. Hili handaki linakuwa katikati ya vifaa viwili vinavyokuwezesha kuingia kwenye tovuti na huduma zingine za mtandaoni kwa faragha na kwa kulindwa dhidi ya wat una mitandao inayokusanya data za watumiaji wa mitandao, wazungu husema unakuwa “invisible.”

HILI HANDAKI LA VPN LINAFANYAJE KAZI?

Hili handaki  linaunda uhusiano baina ya kifaa kimoja na kingine, mara nyingi huwa ni uhusiano wa kifaa unachotumia wewe, mfano: simu, pamoja na seva ya VPN. Hivyo basi, handaki hilo inachukua taarifa zako na kuzisafirisha kwenye mtandao kwa usalama, ikilinda data zako dhidi ya wadukuzi, watoaji huduma za kimtandao, na hata serikali, ili mradi tu uwe umeunganishwa na mtandao wa VPN.

Ili kukufafanulia vyema mambo yanavyofanya kazi, chukulia barabara, mtu akiwa juu kwenye helikopta anaweza kuona magari yanavyoendeshwa barabarani, pamoja na muelekeo wao. Ila pale tu ambapo dereva akaamua kubadilisha njia, atashindwa kuonekana, na ndivyo unavyoweza kumkwepa mtu anaekufuatilia mienendo yako mtandaoni, kama vile watoaji huduma za kimtandao.

VPN INATUMIKA KWA AJILI YA NINI?

VPN ni zana zinazothaminiwa sana ikija kwenye kulinda taarifa zako mitandaoni. Kutokana na hili, watu wengi wameitumia ili kuzuia vizuizi vya mkoa, au nchi, vilivyowekwa na tovuti zingine za mtandao.

Kwa maneno rahisi, VPN ni mfumo ambao hufanya kama kiunga kati ya kompyuta ya mtumiaji na tovuti (au huduma) zilizotumiwa, kuficha utambulisho wao (unganisho, kupitia VPN, linaweza kuonekana kuwa kutoka nchi nyingine), na Kulinda trafiki inayoingia na inayotoka.

SASA VPN INA FAIDA GANI KWAKO?

 

Ukipata kujibu maswali yafuatayo, ndipo utakapoweza kujua kama VPN ina faida au hasara kwako

 

  1. Je unajali faragha yako mtandaoni?

Mtumiaji husajili kwenye mtandao, kwa msaada wa VPN, data zote kwenda / kutoka kwa PC hupitia safu salama. Kwa mfano, unapakua faili. Kwa kukosekana kwa VPN, mtu yeyote anaweza kujua wapi umesajiliwa na ni nani mtoa huduma wako (kupitia IP). Lakini ukiwa na VPN, nafasi hupunguzwa sana, kwani data yako yote imesimbwa kwa njia fiche na IP yako imefunikwa au imechorwa. Yule anaekuwezesha kupata huduma ya intaneti anaweza kuona kila kitu ufanyacho, na anaweza akawa ana kumbukumbu zako za vitu vyo unavyofanya mtandaoni.

  1. Je unapenda au unachukia “censorship’?

Ulishawahi kujaribu kutizama kitu kama vile video katika VEVO na YouTube, au kujaribu kununua bidhaa mtandaoni, na ikakuambia kuwa Kwa mfano, unapenda kutazama video kwenye VEVO. Lakini haipatikani katika nchi yako. Kutumia VPN kupiga IP yako hukuruhusu kutoa IP inayofanana na nchi ambayo upangishaji huu wa video unapatikana.

  1. Unatamani kujikinga dhidi ya wadukuzi?

Wadukuzi sio watu wazuri! Haujui siku wala saa watakayokuamulia, hasa kama wewe ni mzee wa kitonga (Public WiFi), kwani unakuwa umejiweka wazi mbele ya wadukuzi.

Hawa watu wanaweza kupata hata taarifa zako za kiundani kabisa, kabla hauja

  1. Unajali kupunguza gharama na kuokoa pesa yako?

Kutumia VPN kutakusaidia kuokoa pesa kwa kiasi kikubwa sana!

HASARA ZA KUTUMIA VPN NI ZIPI?

Kwa kuwa sasa umeelewa vizuri VPN, matumizi yake, pamoja na faida, tuangaze sasa hasara za kutumia teknolojia hii:

Ubaya kuu wa VPN ni kwamba unganisho, kuwa kwenye mtandao wazi, inakuwa hatari. Na ingawa kesi zilizorekodiwa za utapeli wa VPN ni nadra sana, unahitaji kuelewa kuwa nyongeza inahitajika, kwa mfano, kwa msaada wa teknolojia. Ikumbukwe pia kwamba, inaonekana, NSA ya Amerika ina uwezo wa kupata habari yako kwa kutumia udhaifu mwingine wa PC.

Licha ya umaarufu wao, VPN sio kamili na mipaka iko kama ilivyo kweli kwa teknolojia yoyote. Mashirika yanapaswa kuzingatia masuala kama ya chini wakati wa kupeleka na kutumia mitandao binafsi ya kibinafsi katika shughuli zao: 

  1. VPN zinahitaji uelewa wa kina wa masuala ya usalama wa mtandao na usanidi / usanidi wa makini ili kuhakikisha ulinzi wa kutosha kwenye mtandao wa umma kama mtandao.
  2. Kuegemea na utendaji wa VPN inayotokana na mtandao sio chini ya udhibiti wa moja kwa moja wa shirika. Badala yake, ufumbuzi hutegemea ISP na ubora wa huduma.
  3. Kwa kihistoria, bidhaa za VPN na ufumbuzi kutoka kwa wauzaji mbalimbali hazijawahi sambamba kwa sababu ya masuala yenye viwango vya teknolojia ya VPN. Kujaribu kuchanganya na vifaa vya mechi vinaweza kusababisha matatizo ya kiufundi, na kutumia vifaa kutoka kwa mtoa huduma mmoja huenda si kutoa gharama kubwa za akiba. 

MREJESHO KAMA KIJANA KUHUSU UTUMIAJI WA VPN

VPN ni teknolojia nzuri kama unahitaji kujificha kutoka kwa wadukuzi na wakusanyaji data. Pia itumie kama unataka kuepukana na vikwazo vya kimkoa, au za nchi kwa nchi, kwani VPN itakusaidia kuonekana kuwa unatokea mahala pengine, mbali na hapo ulipo.

Ila tu, kuwa muangalifu kwani utumiaji wa VPN unaweza pia ukawa sio salama, endapo hauna uhakika wa chimbuko la hiyo VPN. Kuwa muangalifu pale unapopakua programu zinazokuwezesha kutumia VPN, na kuhakikisha kuwa imetoka kwenye kampuni za kuaminika, ila wao waliotengeneza hilo handaki, wasitumie taarifa zako halisi dhidi yako.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Detricia Pamba

A Digital Journalist, Content Creation Executive at Mwananchi Communications Ltd and Chief Editor of Mwananchi Scoop. I'm also writes stories around Technology, every Wednesday on Mwananchi Scoop. My other famous segments on Mwananchi Scoop include LISTI and WHO’S HOT.


Latest Post