Maneno 14 ambayo Mwanamke anatamani umwambie

Maneno 14 ambayo Mwanamke anatamani umwambie

Ikija katika maswala ya kuwavutia wanawake, kile kitu ambacho utamtamkia kitakusaidia pakubwa katika azma yako ya kumuwini.

Hakuna ujanja wowote ambayo unatumika bali ni maneno yako. Wanawake ni viumbe ambao ni wasikilivu ilhali wanaume ni viumbe waangalifu, hivyo matumizi yako ya maneno ni silaha nzito ambayo umebarikiwa nayo.

Nikwambie tu ikija katika usikilizi, kila mwanamke huwa tofauti. So itabidi umsome mwanamke kwanza na uyafahamu mambo gani anapenda ili ikija wakati wa kumtamkia maneno itakuwa rahisi kwako kumteka kihisia. Tumeandaa orodha ya maneno ambayo ukiyatumia yapasavyo yatakusaidia kumzuzua mwanamke yoyote awe rafiki yako ama mpenzi wako. Zama nasi.

1 Yuko smarti.

 Hapa hauwezi kukosea wakati utakapomwambia kuwa anapendeza. Unachohitajika ni kumtamkia maneno kama haya wakati ufaao. Unaweza kumweleza sehemu ambayo unaona yuko smarti na utakuwa unamfurahisha wakati wote.

2 Unapenda jazba na msukumo wake
.

 Kama umeona kuwa mwanamke aina hii ana ari na msukumo wa kufanikisha jambo flani basi unapaswa kumpongeza. Kama hana msukumo wowote katika maisha halafu umsifie atashangaa unamsifia na nini. So hakikisha kuwa unampa sifa aina hii kulingana na msukumo wake wa kutimiza jambo fulani katika maisha yake.

3 Unapenda vyenye anavyoishi.

Hapa unamsifia maisha yake yote. Hii ina maana kubwa katika kila kitu cha maisha yake. Wakati unapomtamkia maneno kama haya hakikisha kuwa unakuwa serious na kile ambacho unatamka.

4 Kuwa yeye ni muhimu kwako.

 Kama unajaribu kumuonyesha mwanamke kuwa unamweka kipao mbele katika maisha yako unapaswa umwambie kuwa yeye ni muhimu katika maisha yako. Haya ni matamshi mazito ambayo utamfurahisha na kutamani kuwa na wewe milele.

5 Yeye ni tofauti na wengine.

Kila mwanamke anatamani kuwa spesho. Wanatamani kuwa tofauti na wanawake wengine wale wote. So msifie mwanamke na umwambie kuwa yeye ni tofauti, hakuna mwanamke mwengine ambaye anaweza kufikia kiwango chake. Utafaulu kumuwini.

6 Unajali maslahi yake.

 Wanaume wengi mara nyingi huwa wanashindwa kutamka maneno haya mbele ya mwanamke japo kuwa ni matamshi rahisi ya kusema. Hapa si lazima uingie ndani ueleze sababu zako zote. Kumtamkia maneno kama haya yanatosha kwa mwanamke.

7 Ni mrembo zaidi ya maumbile.

Hapa unatuma ujumbe wakumwambia kuwa yeye kando ya kuwa ni mrembo kimwili, pia ni mrembo ndani yake. Mweleze kinjia ambayo hakutaleta kana kwamba ni mrembo kimaumbile pekee.

8 Anakusisimua bila hata kujaribu chochote.

  Hii ni silaha nzito unapaswa kuitumia kwa kuwa wanawake wengi hupenda kuskia matamshi kama haya. Wanawake wana hisia ndani zao so ukimtamkia maneno kama haya watahisi kujishasha/sifu hivyo wataskia vizuri ndani yao.

9 Kama anataka kuongea uko tayari kumsikiliza.

Hii inaweza kuonekana kama ni mambo ya friend zone lakini ukweli ni kuwa wanawake hupenda kusikilizwa na wapenzi wao. Hii inamaana kuwa uko tayari kutenga nafasi yako spesheli ili uongee naye. Atajihisi tofauti.

10 Utakuwa karibu naye kwa shida na raha
.

Mwanamke anataka utumishi kutoka kwako. Kama una upendo ndani yako kwake, basi atahisi usalama, kukamilika na kupendwa. Hivyo baada ya kusoma hii post spesheli tulioiandika hapa Nesi Mapenzi, unapaswa kumtamkia maneno haya mpenzi wako.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post