Manchester City wapigwa marufuku kusheherekea ushindi

Manchester City wapigwa marufuku kusheherekea ushindi

‘Winga’ wa #ManchesterCity Jack Grealish ameeleza kuwa ‘kocha’ wao Pep Guardiola amewapiga marufuku wachezaji wake kusheherekea ushindi wao kupita kiasi  baada ya ‘klabu’ hiyo kuwafunga #Sevilla kwa mikwaju ya penalti 5-4 kufuatia sare ya 1-1 mjini #Athens, kwenye mchezo wa UEFA Super Cup.

Hata hivyo baadha ya wachezaji wa ‘timu’ hiyo akiwemo Grealish walienda visiwa vya #Ibiza baada ya ushindi huo kisha ‘winga’ huyo aliendelea ku-party kipindi chote cha mapumziko.

Jack ameeleza hayo akiwa katika mahojiano na kituo cha habari cha TNT Sports kwa kusema kuwa, “tumepigwa marufuku kusherekea ushindi hivyo tutarudi nyumbani kujianda na ‘mechi’ zijazo”.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post