Mambo magumu kwa rapa Aiddy, Abwaga manyanga

Mambo magumu kwa rapa Aiddy, Abwaga manyanga

Kufuatiwa na tuhuma za unyanyasaji wa kingono zinazo mkabili mwanamuziki Diddy, sasa msanii huyo amejiuzulu cheo chake cha uwenyekiti katika kampuni ya KEVOLT.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na REVOLT kupitia ukurasa wao wa Instagram kampuni hiyo imedai kuwa imepokea uamuzi huo kwa kuendelea kulenga dhamira yao ya kutoa maudhui yenye maana na yanayoendana na tamaduni zao.

Kampuni hiyo ya REVOLT ilianzishwa mwaka 2013 na Andy Schuo akishirikiana na Diddy kwa lengo la kutoa maudhui ya mwanamuziki huyo kwa njia ya digital cable.

Licha ya hayo Shule za Capital Preparatory ambazo Diddy alikuwa mdhamini katika uendeshaji wa shule na kulipia wanafunzi ada zimetangaza kusitisha uhusiano na mwanamuziki huyo kulinda ustawi na mwenendo wa shule hizo.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post