Mamba mweupe rangi nyeupe apatikana

Mamba mweupe rangi nyeupe apatikana

Siku zote waswahili wanasema ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni, na msemo huu unajidhihirishia kwa mamba huyu mweupe ambaye ni nadra sana kuonekana.

Kulingana na ripoti kutoka kwa mbuga ya wanyama pori ya Gatorland iliyopo Orland, Florida nchini Marekani imeeleza kuwa imempokea rasmi mamba wa kike aina ya leucistic mwenye ngozi nyeupe ambaye ni tofauti kabisa na wenye ulemavu wa ngozi.

Aidha kulingana na ripoti hiyo wameeleza kuwa aina hiyo ya mamba ni nadra kuzaliwa katika karne ya sasa kwa sababu wana hali ya leucism ambayo husababisha kupoteza rangi, iliyozoeleka kwa mamba kuwa nayo.

Mamba huyo aina ya leucistic alitotolewa akiwa na uzito wa gramu 96 na urefu was m 49.

.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post