Mama alivyorudisha tabasamu kwa binti yake

Mama alivyorudisha tabasamu kwa binti yake

Mwanamke mmoja kutoka Utah nchini Marekani aitwaye Daniella amerudisha tabasamu kwa binti yake wa miaka saba aitwaye Gianessa Wride baada ya kubuni njia inayoweza kuwa mbadala wa nywele zake zilizokatika kutokana na ugonjwa.

Binti huyo aligundulika na ugonjwa ujulikanao kwa jina la ‘Alopecia’, ambao hauna tiba unaomfanya mtu apoteze nywele zote, ndipo mama huyo akaamua kupamba kichwa cha Gainessa kwa kutumia vito (stone) za kung’aa.

Ubunifu huo unatajwa kuwa ni wakipekee kutokana na binti huyo kuwa na furaha hata akiwa shuleni huku akijiona sawa kama watu wengine.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BuurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post