Kondoo wazidiwa baada ya kula bangi

Kondoo wazidiwa baada ya kula bangi

Kundi la kondoo nchini Ugiriki kwenye mji wa Almyros limevamia nyumba ya kuhifadhia mimea na kula bangi  zilizokuwa zimehifadhiwa kwa ajili ya matibabu.

Inadaiwa kuwa kondoo hao walikuwa wakitafuta sehemu ya kujihifadhi  kutokana na mafuriko baada ya tukio la Storm Daniel kusababisha mafuriko makubwa nchini Libya, Turney, Bulgaria, pamoja na Ugiriki.

Ndipo katika nyumba hiyo walikutana na mimea hiyo iliyokuwa imetunzwa kwa ajili ya kutengenezea tiba.

Hata hivyo mmiliki wa kondoo hao alipatikana na kudai, baada ya tukio hilo kutokea aliona mifugo yake ikizidiwa na ikiruka juu kuliko kondoo wengine ndipo akagundua kuwa mmea huo utakuwa umewalewesha.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post