Guinea yathibitisha mlipuko wa ugonjwa wa Marburg

Guinea yathibitisha mlipuko wa ugonjwa wa Marburg

Guinea ya Ikweta imethibitisha mlipuko wa kwanza kabisaa wa ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Marburg.

Waziri wa afya nchini humo Mitoha Ondo'o Ayekaba, amesema jana Jumatatu kwamba watu wasiopungua tisa wamekufa kutokana na ugonjwa huo katika mkoa wa Kie-Ntem.

Shirika la afya duniani, WHO pia limethibitisha mlipuko huo na kusema timu za wataalamu zimetumwa kufuatilia watu waliotangamana na waathirika, kuwatenga wale wanaoonesha dalili na kutoa huduma.

Dalili kuu za ugonjwa huo mpaka sasa zinahusisha uchovu, matapishi yaliochanganyika na damu na kuharisha.

Kirusi cha Marburg kinahusiana na Ebola ambayo ilisababisha maafa makubwa katika milipuko kadhaa ya huko nyuma barani Afrika.

Hakuna chanjo zilizoidhinishwa au dawa za kutibu ugonjwa wa Marburg, lakini tiba ya kuongeza maji mwilini kupunguza dalili inaweza kuongeza nafasi ya kupona kwa mgonjwa.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post