Fabregas awa kocha mkuu

Fabregas awa kocha mkuu

Mchezaji wa zamani wa ‘timu’ ya #Arsenal, Barcelona na Chelsea, #CescFabregas ameteuliwa kuwa ‘Kocha’ Mkuu wa ‘klabu’ ya #ComoFC inayoshiriki ‘Ligi’ daraja la pili nchini Italy.

Nyota huyo wa zamani wa ‘timu’ ya taifa ya #Uhispania alikuwa ‘kocha’ wa kikosi cha vijana cha ‘klabu’ hiyo na sasa atakuwa ‘kocha’ wa kikosi cha wakubwa ikiwa ni uzoefu wake mpya kwenye kikosi cha kwanza.

Kiungo huyo wa zamani ni miongoni mwa wanahisa wa ‘klabu’ hiyo inayomilikiwa na kampuni ya #Djarum.

.

.

.

#MwananchiScoop

#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post