Darasa kuburuzwa mahakamani

Darasa kuburuzwa mahakamani

 

Mmmmmmmh! Kwahiyo mnataka kutufanyia mambo ya mzee wa buga, basi bwana kwa taarifa zilizotufikia ni kwamba msaanii wa hip hop Darasa aburuzwa mahakamani baada ya kutotokea katika show yake jijini Mbeya

Mbeya .Mahakama ya Wilaya ya Mbeya  imepokea  shauri la madai  dhidi ya  Msanii wa kizazi kipya Shariff Thabeet maarufu  (darasa) na Daniel Mwailubi  Mmiliki wa Mwailubi Lounge kwa madai ya kuvunja mkataba na kuwadanganya  wananchi kufanya tamasha la beer Festive Season 28 lililotakiwa kufanyika Julai 30 mwaka huu.

Shauri hilo  limewasilishwa na Mwanasheria wa Kampuni Baistar Advocate ya Jijini Mbeya dhidi ya wateja wake  Arnold Francis Kisheni na Seiph Mussa Wembe mbele ya Hakimu Mkazi  Happiness Chuwa  mnamo Agosti 24 mwaka huu.

Mbwilo ameliambia Mwananchi leo Jumatatu Agosti 29 ,2022 kuwa awali shauri hilo lilipowasilihwa Mahakama mdaiwa wa kwanza Danny Mwailubi  amepatiwa nakala ya madai na kutakiwa kupeleka utetezi wake Mahakamani Septemba 5 mwaka huu  huku msanii Shariff Thabeet (darasa) wakiendelea kumtafuta .

 Amesema kutokana na hadha waliyoipata na usumbufu kwa wateja wake wamewasilisha madai ya fidi a Sh  71.4 Milioni ikiwa ni madai halisi huku 200 Milioni fidia ya madhara waliyoyapata

Mbwiro ameeleza kuwa  mnamo Julai 29 mwaka huu  walalamikaji  wakiwa Mpanda Mkoa wa Katavi waliona tangazo kwenye akaunti za  Instagram za wadaiwa wakitangaza kuwepo kwa tamasha la Beer Festival Season 28  .

 

Tangazo hilo ambalo liliambatana na picha ya msaanii ,Sharif Thabeet maarufu kama ''darasa'' kwa kiingilio cha 10,000 na beer  ambalo lililotakiwa kufanyika Julai 30 mwaka huu na badala yake kuvunja makubaliano baina ya wadaiwa  na wateja kwa msanii hiyo kutopanda stejini kama ilivyokuwa makubaliano.

''Wateja wangu walisafiri kutoka Mkoa wa Katavi kuja kushuhudia tamasha hilo lakini walikaa  mpaka alfajiri pasipo msanii kupanda stejini na wala Mmiliki wa Mwailubi Lounge kuwaeleza chochote ''amesema.

Amesema kuwa kutokana na madhara waliyopata   wamefungua kesi ya madai ya  Sh 71.4 Milioni kama madai halisi huku Sh 200 Milioni fidia ya madhara (General Damages) pamoja na kuwataka kuomba msamahausio na masharti na kulipa gharama za uendeshaji wa kesi Mahakamani.

Kwa upande wake Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya Mkoa wa Mbeya ,Happiness Chuwa amepanga kusikilizwa kwa shauri hilo namba 25/2022 Septemba 5 mwaka huu huku wakimtaka mmiliki wa Mwailubi Lounge apeleke utetezi wake Mahakamani ikiwa ni pamoja na kumtafuta msanii wa Kizazi kipya maarufu kama Darasa.

Amewataka wasanii na waendesha matamasha wajue sheria haipo kimya kwani ipo na inalinda upande zote mbili kwa walioandaa na waliohudhuria .






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Detricia Pamba

A Digital Journalist, Content Creation Executive at Mwananchi Communications Ltd and Chief Editor of Mwananchi Scoop. I'm also writes stories around Technology, every Wednesday on Mwananchi Scoop. My other famous segments on Mwananchi Scoop include LISTI and WHO’S HOT.


Latest Post