Cardi B, Offset wafikishwa mahakamani kisa kodi

Cardi B, Offset wafikishwa mahakamani kisa kodi

'Rapa’ kutoka nchini Marekani Offset na mkewe Cardi B wafikishwa mahakamani baada ya kushindwa kulipa kodi katika nyumba waliyokuwa wakiishi mwaka 2022.

Kwa mujibu wa Tmz News imeripoti kuwa wanandoa hao waliondaka katika nyumba hiyo iliyopo ‘Beverly Hills’ bila ya kurudisha nyumba kwa wamiliki.

Aidha kupitia hati hizo zilizopelekwa mahakamani zimeeleza kuwa wamiliki wanadai fidia kutokana na nyumba yao kupata uharibifu wa mali unaogarimu dola 85,000.

Drama hizo za kudaiwa kodi zinakuja baada ya uhusiano wa Cardi B na Offset kuvunjika ambapo Cardi alidai kuwa mumewe amemsaliti.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post