Card B akanusha kumcheat mumewe

Card B akanusha kumcheat mumewe

Rapa kutoka nchini Marekani Cardi B amekanusha madai ya kumcheat mume wake Offset, hii ni baada ya mpenzi wake huyo kupost insta story akidai kusalitiwa na mkewe.

Kupitia twitter space ya mwanadada Cardi B ameweka wazi kwa kukanusha madai hayo akieleza kuwa…

“Tafadhali sana acha kujifanya mpuuzi, kwanza kabisa huwezi kunituhumu kwenye makosa ambayo unajua kabisa wewe ndio mwenye hatia na najua kuwa kwako ni rahisi kunilaumu kwa kila kitu” aliendelea kwa kueleza

‘Sikilizeni, msimzingatie huyo mshamba, nahisi kuna muda kuna watu wanasahau kuwa mimi ni Cardi B, ningekuwa nimelala na mtu kila mtu angejua mimi sio wakulala na kila mtu, kwahiyo usinichezee kabisa, ni hayo tu nilikuwa nayo ya kusema” amesema rapa huyo






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post