BREAKING NEWS: Masoud Abdallah Afariki Dunia

BREAKING NEWS: Masoud Abdallah Afariki Dunia

Kwa masikitiko makubwa, aliyekuwa Mbunge wa Mtambile, Nd. Masoud Abdallah Salim amefariki dunia leo katika hospitali ya rufaa ya Mkoani iliyopo huko Pemba, Zanzibar.

Taarifa za kifo cha mwanasiasa huyo zimethibitishwa na Katibu wa Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa ACT Wazalendo, Salim Bimani.

Salim amekuwa mbunge wa Mtambile kupitia CUF kuanzia mwaka 2003 – 2020 na katika Bunge lililopita alikuwa mjumbe wa kamati ya ulinzi na usalama kabla ya kuhamia ACT Wazalendo mwaka 2020 kumfuata Maalim Seif Sharif Hamad ambaye alivuliwa uanachama wa CUF na kwenda ACT Wazalendo.

Taarifa zaidi zitakujia baadae.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Detricia Pamba

A Digital Journalist, Content Creation Executive at Mwananchi Communications Ltd and Chief Editor of Mwananchi Scoop. I'm also writes stories around Technology, every Wednesday on Mwananchi Scoop. My other famous segments on Mwananchi Scoop include LISTI and WHO’S HOT.


Latest Post