Ageuka kichekesho akiwakimbia polisi kwa gari la ‘gofu’

Ageuka kichekesho akiwakimbia polisi kwa gari la ‘gofu’

Mwanamume mmoja kutoka San Fernando ajikuta akigeuka kichekesho wakati akijaribu kuwakimbia maafisa wa polisi  wakiwa kwenye msako.

Kufuatia video zinazosambaa zinamuonesha mwanaume huyo akiwa anawatoroka polisi kwa kutumia gari litumikalo kwenye mchezo wa ‘gofu’, huku mkono mmoja akiwa anatumia kuendesha gari hilo na mwingine akiutumia kumshikilia mbwa wake.

Mwanaume huyo anadaiwa kuiba gari hilo la ‘gofu’ alilotumia kukimbia nalo japo kuwa mbio zake hazikuzaa matunda kwani aliweza kukamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi huku mbwa wake akiwa amerudishwa kwenye familia ya mwanaume huyo.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post