Afariki baada ya kutumia dawa za kupunguza uzito

Afariki baada ya kutumia dawa za kupunguza uzito

Mwanamke mmoja kutoka nchini Austalia aliyejulikana kwa jina la Trish Webster, amefariki dunia baada ya kutumia dawa za kupunguza uzito ili aweze kuvaa gauni la ndoto yake katika harusi ya binti yake.

Dawa hizo ziitwazo Ozempic zinadaiwa kumsaidi mwanamama huyo kupungua kwa haraka kilo 15 ndani ya miezi mitano  lakini zilimsababishia ugonjwa wa kupooza kwa tumbo (gastroparesis) uliopelekea kusababisha kifo chake.

 Ozempic ni dawa iliyoidhinishwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini Marekani kwa watu walio na kisukari cha aina ya 2 na imekuwa ikitumiwa kama dawa ya kupunguza uzito duniani kote.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post