Abby Chams aandika historia

Abby Chams aandika historia

Binti wa kitanzania ambaye pia ni mwanamuziki Abby Chams ameandika historia baada ya kupata bahati ya kuwakilisha mabinti wa Tanzania pamoja na Afrika kwa ujumla katika Talk Show kubwa nchini Marekani inayojulikana kwa jina la Kellyclarkson show.

Abby amepata bahati ya kuzungumza kwenye talk show hiyo kubwa duniani katika siku ya mtoto wa kike duniani ambapo alipata nagasi hiyo kutokana na jitihada zake za kuinua mabinti kupitia program yake ya teentalk with abby.

Hata hivyo Abby amefunguka na kusema hakutegemea kuwa ipo siku ataonekana katika show hiyo hivyo amejiona kuwa anachokifanya kinathamani na kuigusa jamii.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post