Mipango ya Simba kimataifa

Mipango ya Simba kimataifa

Akizungumza na waandishi wa habari Afisa wa Habari na Mawasilino wa 'klabu' ya Simba, Ahmed Ally kuelekea ‘mechi’ ya kufuzu hatua ya makundi dhidi ya ‘klabu’ Power Dyamos ya nchini Zambia amethibitisha kuwa ‘klabu’ yao inapanga kuweka kambi ya muda mfupi nchini, kuelekea mchezo wao huo wa ugenini, mwezi Septemba mwaka huu.

Aidha ‘timu’ hiyo kwa mujibu wa Afisa huyo pia imepanga kucheza ‘mechi’ mbili za kirafiki, moja kutoka ndani na nyingine kutoka nje ya mipaka ya Tanzania kwa ajili ya kujianda na mchezo dhidi ya Power Dynamos.

Na akiwathibitishia mashabiki wa Simba  kuwa 'Winga' kutoka Ivory Coast, Aubin Kramo pamoja na Beki Henock Inonga, wamerejea kikosini baada ya kuwa nje wakisumbuliwa na majeraha alieleza kwa sasa wako ‘fiti’ na wanaendelea na mazoezi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post