Kocha Klopp atimiza ndoto ya shabiki

Kocha Klopp atimiza ndoto ya shabiki

‘Kocha’ wa ‘klabu’ ya #Liverpool, #JurgenKlopp ametimiza ndoto ya shabiki wa ‘timu’ hiyo raia wa #Ireland kwa kumualika kwenye viwanja vya mazoezi na kumkutanisha na baadhi ya wachezaji akiwemo #MohamedSalaha.

Shabiki huyo aitwaye #DaireGorman, alizaliwa akiwa na ulemavu wa viungo, kitaalamu huitwa #CrommelinSyndrome alipata umaarufu Septemba mwaka huu baada ya video zake ku-trend mitandaoni akiwa analia wakati wimbo maalumu wa ‘klabu’ hiyo wa 'You'll Never Walk Alone' ukiimbwa kabla ya mchezo wao dhidi ya Aston Villa.

‘Klabu’ hiyo ime-share video kupitia mitandao ya kijamii ikimuonesha shabiki huyo aliyeongozana na familia yake ndani ya viwacha vya mazoezi vya Liverpool ambapo alifanikiwa kukutana na baadhi ya wachezaji wa ‘klabu’ hiyo na kupiga nao stori.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post