Jason akanusha kuvunjika kwa ndoa yake siku ya harusi

Jason akanusha kuvunjika kwa ndoa yake siku ya harusi

Jason Alexander, mume wa zamani wa mwimbaji kutoka #Marekani, #BritneySpears akana madai ya kulewa siku ya harusi yao, badala yake, amesisitiza kuwa siku hiyo alikuwa amechoka sana.

Jason, ambaye alifunga ndoa na Britney mwaka 2004 kabla ya kupata talaka, amewambia TMZ kuwa wasomaji wasiamini neno lolote la Britney kuhusu ndoa yao katika kitabu chake kipya, cha ''The Woman in Me''.

Britney katika kitabu chake hicho amefichua kuwa yeye na Alexander waligombana mwaka 2004 baada ya usiku wa ndoa yao huko Las Vegas.

Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 45 sasa anatamba wimbo wake wa ‘Mind your business’ aliouachia miezi mitatu iliyopita.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post