Idris Sultan apata shavu Marekani

Idris Sultan apata shavu Marekani

Muigizaji na mchekeshaji maarufu hapa nchini, Idris Sultan  ametangazwa rasmi kuhost katika tuzo za African Entertainment Awards USA (AEAUSA).

Tuzo zinatarajiwa kufanyika Desemba 26 mwaka huu huko Marekani na Idris kupitia ukurasa wake wa Instagram amethibitisha kuwa yeye ni miongoni mwa watakaosherehesha katika tuzo hizo.

“Bigger Better and stronger. Idris Sultan will be hosting the 7th Annual African Entertainment Awards USA with Nancy Isime on December 26th 2021,” ameandika Idris

Miongoni mwa wasanii wanaowania tuzo hizo ni Diamond Platnumz, Alikiba, Harmonize, RosaRee, NavyKenzo, Rayvanny, Zuchu, Mbosso, MimiMars, Nandy, Weusi pamoja na Macvoice kutoka NLM.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm


Latest Post