Buya amtuma mdogo wake amuwakilishe kwenye ndoa yake

Buya amtuma mdogo wake amuwakilishe kwenye ndoa yake

Alooooooooh! Kumbe haya mambo bado yapo bwana ya watu kuoleana yaani kumuwakilisha mtu katika ndoa yake pindi yeye mwenyewe muhusika anapokuwa mbali.

Basi bwana Mchezaji wa Sierra Leon πŸ‡ΈπŸ‡± Mohamed Buya hakushiriki kwenye sherehe ya harusi yake kwa sababu alikwenda kuwahi usajili na klabu yake mpya ya Malmo ya nchini Sweden.

Buya alimtuma mdogo wake Baydoun asimame na kumuwakilisha  kama Bwana harusi kwa niaba yake

Baada ya ndoa hiyo Buya kupitia mtandao wake wa kijamii wa Twiter alionesha furaha yake kwa kuandika “Nimeoa mchumba wangu, mke na rafiki yangu wa karibu leo!!! Ni binadamu wa ajabu sana!!! Na ni baraka iliyoje!!! Mrs SBT Suad Baydoun, Siwezi kusubiri kufurahia maisha na wewe pamoja sobot” ameandika Mohamed Buya

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post