Borisa Simanic apoteza figo baada ya kupigwa kiwiko uwanjani

Borisa Simanic apoteza figo baada ya kupigwa kiwiko uwanjani

Mchezaji wa mpira wa kikapu kutoka nchini Serbia, Borisa Simanic amelazimika kuondolewa figo baada ya kuumia wakati wa mchezo wa Kombe la Dunia la FIBA kwa kupigwa kiwiko na mchezaji mwenzie kutoka Sudan Nuni Omot.

Borisa mwenye umri wa miaka 25 alipata majeraha hayo wakati akimlinda mchezaji huyo asiweze kuifunga timu yake.

Kwa upande wa mchezi aliyempiga kiwiko Omot alitoa taarifa akisema hakuwa na nia yoyote ya kumuumiza Simanic na anasikitishwa na jambo hili kutokea kwake, hivyo basi anamuombea  mchezaji mwenzake apone na aweze kurejea mchezoni.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post