Bernard Morrison aitingisha Simba

Bernard Morrison aitingisha Simba

YANGA imekamilisha usajili wa mshambuliaji kutoka Asec Mimosas, Stephano Ki Aziz wakati huo huo taarifa za ndani ya klabu hiyo zinaeleza imekamilisha usajili wa Benard Morrison kutoka Simba.

Morrison atachelewa kutambulishwa kutokana na mkataba wake na Simba kumalizika Agosti 30, mwaka huu, siku chache kabla ya msimu ujao kuanza wakati huo hadi mechi ya Ngao ya Hisani itakuwa imechezwa.

Taarifa kutoka ndani ya Simba zinaeleza Morrison ametuma maombi kwa njia mbalimbali, ujumbe mfupi wa maneno wa simu, barua pepe, kupiga simu na kuzungumza na viongozi wa juu ili wampe barua inayoonyesha yupo huru.

Morrison amewaomba mabosi wake ambao hivi karibuni walimtakia kila la heri kwenda kutatua matatizo ya kifamilia kumpatia barua hiyo akieleza kwamba kuna timu kutoka nchi mbalimbali zinamtaka.

Kiongozi mmoja wa Simba alisema Morrison amewafuata na kuwaeleza amepata ofa kutoka timu kama Raja Casablanca ya Morocco na Qatar.

“Baada ya kutueleza timu zinazotaka kumsajili akatuomba tumpatie ‘release latter’ ili akamalizane nao na kuanza maisha mapya huko. Tumemjibu hizo timu zinazomtaka zitutumie barua rasmi ya kuonyesha nia hiyo nasi tutakuwa tayari kuwapatia,” alisema kiongozi huyo.

Imeandaliwa na Thobias Sebastian, Mwanaspoti






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Detricia Pamba

A Digital Journalist, Content Creation Executive at Mwananchi Communications Ltd and Chief Editor of Mwananchi Scoop. I'm also writes stories around Technology, every Wednesday on Mwananchi Scoop. My other famous segments on Mwananchi Scoop include LISTI and WHO’S HOT.


Latest Post