Mwanamuziki Harmonize amekanusha kauli ya aliyekuwa msanii wake Ibraah ya kumdai kiasi cha Sh 1 Bilioni ili aweze kutoka katika lebo ya ‘Konde Gang’.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Harmonize ametoa maelezo kuhusu sakata hilo huku akiweka wazi hajui kuhisiana na andiko la Ibraah katika mitandao ya kijamii la kumdai Sh 1 Bilioni.
“Niko hapa kuadress jambo linalo muhusu mdogo wangu Chinga, kwanza kabisa nikiri alinitumia meseji na kuniomba kwamba anataka kuondoka kwenye lebo akawe Independent Artist nilimkubali na kumtakia kila la kheri nikamwambia kaa chini na viongozi wa Konde Gang muone mnafanyaje.
“Mkataba wake unasema endapo anataka kuondoka na kununua haki miliki zake za nyimbo alizozifanya hata zile alizozifanya na mimi ili ziwe za kwake muda wote, ziwe zinaingiza pesa kwake inatakiwa alipie kuzinunua hicho kiasi cha pesa kilichotajwa kwenye mkataba ambao alisaini miaka minne iliyopita na kampuni ya Konde Music,”amesema Harmonize
Afunguka kuhusu kumdai Sh 1 Billioni
“Sijui nini kimetokea kwake badaye akaja kusema kwenye social media kwamba nimemdai kiasi cha Sh 1Bilioni nikiri kwamba sijamdai pesa hiyo nisingependa tena pesa yangu ije kunichafua mimi mwenyewe. Kwasasa ni msanii huru namtakia kila la kheri promota mkiwa na show muiteni apate riziki aisaidie familia yake,”amesema Konde Boy
Aidha akizungumza kuhisiana na ishu ya BASATA kutoitikia wito huo ameeleza kuwa aliliwasilisha kwa menejimenti yake ili imuwakilishe.
“Lakini pia kuhisiana na Basata nilipata wito na niliomba menejimenti yangu iniwakilishe nilitaka kujua tatizo nini kwa sababu mazungumzo yangu na Bwana Chinga sikutegemea yangeweza kufika Basata.
“Viongozi wa Basata wanapataje muafaka lakini wakanambia waliyonambia so far nisingeweza kuyashare sasahivi. Mimi sikuona haja ya kusuluhisha na mdogo wangu au msanii ambaye nimemtengeneza mimi mwenyewe sikuona haja ya kutengeneza sitofahamu na tahaluki,”amesema Konde Boy
Aidha ameongezea kwa kueleza “Nimemruhusu aende akafanye akafanye mziki wake and make sure mnamsapoti pia. Na kuhusu kauli yake ya nimemuita chumbani it’s sad na sio kwamba sijui kuna baadhi ya watu wanaweza kuamini kwamba ni kweli lakini sina namna kwasababu mtoto akiunyea mkono huwezi kuukata.
“Kwanza nimemuachia Mungu, pili nimemsamehe na mwisho namuombea mimi sihitaji msamaha wowote kutoka kwake akiona kunahaja ya kuomba msamaha ni sawa akiona hakuna haja pia ni sawa,”amemalizia Harmonize

Leave a Reply