Pakistan: Watu 18 wa familia moja wafariki katika ajali ya basi

Pakistan: Watu 18 wa familia moja wafariki katika ajali ya basi

Mamlaka nchini Pakistan zimefahamisha kuwa watu 18 wa familia moja wakiwemo watoto 12 wamefariki baada ya basi waliyokuwa wakisafiria kuteketea kwa moto kutokana na hitilafu ya mfumo wa umeme.

Afisa wa polisi wa eneo hilo Javed Baloch amesema baadhi ya miili imeharibiwa na moto kiasi cha kutotambulika. Basi hilo lilikuwa limewabeba watu 50 wenye uhusiano wa kindugu wakitokea mji wa kusini wa Karachi kuelekea Jimbo la Sindh.

Familia hiyo ilihamia Karachi mwezi Agosti baada ya mji wao wa "Khairpur Nathan Shah" kukumbwa na mafuriko makubwa yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu 2,000 nchini humo.

Barabara mbovu, magari yasiyotunzwa vizuri na mfumo duni wa usalama barabarani husababisha kila mwaka ajali nyingi nchini Pakistan na kulingana na takwimu za serikali,ajali hizo husababisha maelfu ya vifo.

Chanzo DW






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post