Hivi hapa vipengele vya wanaowania tuzo za TMA

Hivi hapa vipengele vya wanaowania tuzo za TMA

Ikiwa jana Septemba 3, 2024 dirisha la kuwapigia kura wasanii watakaowania Tuzo za Muziki Tanzania (TMA) lilifunguliwa, hivi ndivyo vipengele 17 vinavyoshindaniwa ambavyo vimetajwa na kamati ya waandaji wa tuzo hizo inayoongozwa na Mwenyekiti wake David Minja na Makamu Mwenyekiti Seven Mosha.

Kipengele cha Mwanamuziki Bora Wa Kiume Wa Mwaka wanaowania ni Marioo wimbo wa ‘Shisha’, Diamond ‘Shu’, Harmonize ‘Single Again’, AliKiba ‘Sumu’ na mwisho ni Jay Melody na wimbo wa ‘Nitasema’.

Na kipengele cha Mwanamuziki Bora wa Kike Wa Mwaka wanaowania ni Zuchu ‘Honey’, Anjella ‘Blessing’, Malkia Leyla Rashid ‘Watu na Viatu’, na Nandy ‘Falling’.

Mwimbaji Bora wa Kiume wa Bongo Fleva wa mwaka ni kipengele ambacho wanaoshindania ni Diamond ‘Yatapita’, Jay Melody ‘Sawa’, Alikiba ‘Mahaba’, Marioo ‘Love song’ na Harmonize ‘Single Again’.

Mwimbaji Bora wa Kike wa Bongo Fleva wa Mwaka wanaowania ni Zuchu ‘Naringa’, Appy ‘Watu feki’, Nandy ‘Falling’, Phina ‘Sisi ni wale’ na Anjella ‘Blessing’.

Wimbo Bora wa Ushirikiano wa Mwaka wanaochuana ni Alikiba ft Marioo ‘Sumu’, Mbosso ft Chley ‘Sele’, Abigail Chams ft Marioo ‘Nani’, Jux ft Diamond ‘Enjoy’ na Diamond ft Koffie Olomide ‘Achii’.

Katika kipengele cha Albumu Bora ya Mwaka walioingia katika mchuano huo ni Abigail Chams ‘5’, D Voice ‘Swahili Kid’, Navy Kenzo ‘Most People Want This’, Harmonize ‘Visit Bongo na Rayvanny ‘Flowers III.

Aidha kwenye kipengele cha Mwanamuziki Bora Chipukizi wa Mwaka wanaoshindanishwa ni Xouh ‘Lalala’, Chino Kidd ‘Gibela’, Appy ‘Watu feki’, Mocco Genius ‘Mi Nawe’ na Yammi ‘Namchukia’.

Wimbo Bora wa Hip Hop wa Mwaka wanaochuana ni Rapcha ‘Uongo’, Country Wizzy ‘Current Situation’, Young Lunya ‘Stupid’, Stamina ft Bushoke ‘Machozi’ na Joh Makini ‘Bobea’.

Huku wanaowania Mwimbaji Bora wa Hip Hop ni Young Lunya ‘Stupid’, Kontawa ‘Dunga mawe’, Stamina ‘Machozi’, Joh Makini ‘Bobea’ na Rosa Ree ‘Mama Omollo’.

Mtozi Bora wa muziki wa Hip Hop wa mwaka wanaoshindanishwa ni Black Beats ‘Warrior’, S2kizzy ‘Maokoto’, Ommydaddy ‘Wanangu Kibao’, Ringle Beatz ‘Tribulation’ na Dupy Beatz ‘Mr. Christmas part 5’.

Upande wa DJ Bora wa Mwaka wanaoshindania ni Dj D Ommy, Dj Seven Worldwide, Dj Shana Mnyamwezi, Dj, Dj Hijab na Dj Mamie.

Katika kipengele cha Mtumbuizaji Bora wa Kike wa Mwaka, waliotajwa ni Zuchu (Nani remix), Phina (Do Salale), Abigal Chams (Milele) na Da Princess (Lolo).

Kwa upande wa Mtumbuizaji Bora wa Kiume wa Mwaka wanaowania ni pamoja na Mbosso ‘Sele’, Christian Bella ‘Tamu’, Harmonize ‘Single Again’, Alikiba ‘Sumu’ na Diamond ‘Shu!’.

Mtunzi Bora wa Muziki wa Dansi wa mwaka wanaowania ni Master Keys, Dad One Touch, Erasto Mashine na Christian Bella. Aidha Mwandishi Bora wa Mwaka waliotajwa ni Mbosso, Dulla Makabila, Thabiti Abdul, Jay Melody na Marioo.

Mtozi Bora wa Muziki wa Bongo Fleva wa Mwaka wanaoshindanishwa ni pamoja na Ibrah Jacko, Aloneym, Trone, S2kizzy na Mr. L. huku wanaowania tuzo ya Mtonzi Bora wa Muziki wa mwaka wakiwa ni S2kizzy, Mr.LG, Lizer, Thabit Abdul na Trone.

Mwongozaji Bora Video ya Muziki wa Mwaka Hanscana ‘Maokoto’, Nicklass ‘Dunga Mawe’, Ivan ‘Sele’ , Folex ‘Achii’ na Director Wayan ‘Huku’.

Mwanamuziki Bora wa Nyimbo za Asili, wanaowania ni Elizabeth Maliganya ‘Boda Boda’, Erica Lulakwa ‘Aragoba’, Sinaubi Zawose ‘Pesa’, Ngapi Group ‘Berita’ na Wamwiduka Band ‘Usizime Muziki’.

Huku wanaowania Wimbo bora wa Asili wa Mwaka ni Sinaubi ‘Pesa’ Man Fongo & Nyati Group ‘Sauti ya Kumoyo’, Erica Lilakwa ‘Aragoba’, Wazawa Music Band ‘Muziki hauna mwenyewe’ na Wamwiduka Band ‘Usizime Muziki’.

Mwimbaji Bora wa Muziki wa Dansi wa Mwaka wanaoshindanishwa ni Christian Bella ‘Kanivuruga’, Melody Mbassa ‘Hellena’, Papi Kocha ‘Jela ya Mapenzi’, Charlz Baba ‘Mmbeya’ na Sarah Masauti ‘Popo’.

Wimbo Bora Dansi Wa Mwaka wanaowania ni Diamond ft Koffie Olomide na ngoma ya ‘Achii’, Melody Mbassa ‘Nyoka’, Malaika Band ‘Kanivuruga’ na Twanga Pepeta ‘Mmbea’.

Kwenye upande wa Mwanamuziki Bora wa Dancehall wa Mwaka waliotajwa ni Dj Davizo ‘Dancehall’, Baddest 47 ‘Zagamua’, Appy ‘Mr Hater’ na Bayo The Great ‘Nakupenda’. Huku upande wa Wimbo Bora wa Dancehall wa Mwaka wanaoshindanishwa ni Planner ‘You’, Bayo The Dreat ‘Nakupenda’, Dj Davizo ‘Dancehall’, Appy ‘Mr Hater’ na Baddest 47 ‘Zagamua’.

Mbali na vipengele hivyo pia kipo kipengele cha Mwanamuziki Bora wa Reggae wa Mwaka wanao wania ni Akilimali ‘Africa Mama’, Dipper rato ‘Grateful’, Dimateo Zion ‘Rhymes ToNight’, Ras Nono ‘Andika’ na Warriors From The East ‘Wewe’.

Wimbo Bora wa Reggae wa Mwaka wanaoshindanishwa ni Warriors From The East ‘Wewe’, Akilimali ‘Africa Mama’, Dimateo Zion ‘Rhymes ToNight’ Mr. Kamanzi ‘Give And Thanks’ na Paul Mihambo ‘Salamu zako’.

Katika upande wa Taarabu vipo vipengele vitatu ambayo ni Mtuzi bora, mwimbaji bora na wimbo bora ambapo wanaowania kwenye Mtunzi Bora wa Muziki wa Taarabu wa Mwaka ni Father Mauji ‘Umenibamba’, Bob Rama ‘Nkurumbi’, Bbu Juha ‘Kisaka’, Thabit Abdul ‘DSM Sweetheart’ na Mfalme Mzee Yusuph ‘Sina Wema’

Mwimbaji Bora Wa Taarabu wa Mwaka waliotajwa ni pamoja na Salha ‘DSM Sweetheart’, Mwinyimkuu ‘Bila yeye sijiwezi’ , Malkia Leyla Rashid ‘Watu na Viatu’, Amina Kidevu ‘Hatuachani’ na Mwansiti Mbwana ‘Sina Wema’.

Huku wanaowania katika kipengele cha Wimbo Bora wa Taarabu wa Mwaka ni Malkia Leyla Rashid ‘Watu na Viatu’, Salha ‘DSM Sweetheart’ , Mwansiti Mbwana ‘Sina Wema’, Mwinyimkuu ‘Bila yeye sijiwezi’ na Amina Kidevu ‘Hatuachani’.

Katika upande wa kipengele cha Mtanzania Anayeipeperusha Vyema Bendera ya Tanzania Kimataifa (Tanzania Global Icons Award) wanaowania ni mchezaji wa mpira wa miguu Mbwana Samatta, mwanamitindo Flaviana Matata, wanasarakasi Ramadhan Brothers, pamoja na Anisa Mpungwe na Clara Luvanga.

Pia kuna kipengele cha Video Bora ya Muziki ya Mwaka ambapo wanaowania ni pamoja na Billnass ‘Maokoto’, Mbosso ‘Sele’, Zuchu ft Innos B ‘Nani Remix’, Diamond ft Koffie Olomide na ngoma ya ‘Achii’, na Harmonize ‘Single Again remix’.

Aidha Wimbo Bora wa Mwaka wanaotoana jasho kwenye kipengele hicho ni pamoja na Zuchu ‘Honey’, Harmonize ‘Single again’, Jux ft Diamond ‘Enjoy’, Lava Lava ‘Tajiri’ na Diamond ‘Shu!’.

Huku kipengele cha mwisho ya Best Song East West and Southern Afrika wanaowania ni Libianca ‘People’, Qing Madi ‘American Love’, Asake ‘Lonely at the top’, David oft Musa Keys ‘Unavailable’ na Tyler ICU and Tumelo ft Dj Maphorisa ‘Mnike’

Tuzo hizo za muziki Tanzania (TMA) zinatarajiwa kutolewa Septemba 29, 2024 huku dirisha la kupiga kura likifungwa Septemba 28, 2024.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post