Walimu wakamatwa kufuatiwa video chafu ya wanafunzi

Walimu wakamatwa kufuatiwa video chafu ya wanafunzi

Polisi nchini Kenya wamewakamata walimu sita wa shule ya msingi katika eneo la magharibi mwa nchi, kufuatia clip ya video iliyotrend mitandaoni ikiwaonyesha wanafunzi wakiiga kitendo cha ngono huku wakiwatazama.

Vyombo vya habari nchini humo vinaripoti kuwa walimu hao wa Nyamache, katika jimbo la Kisii, walikamatwa baada ya maafisa wa Wizara ya Elimu kutazama video hiyo na kutoa malalamiko.

Katika video hiyo, watu wazima wanaoshukiwa kuwa walimu wanasikika wakijadiliana na kucheka kwa sauti huku mtu akiwarekodi wavulana wanne ambao wamevalia sare za shule.

Ripoti ya polisi ilibainisha kuwa clip hiyo "kuwafichua wanafunzi katika kitendo kichafu" ilionekana kuwa ilitoka shuleni. Ilisema sita waliokamatwa walikuwa wakisaidia katika uchunguzi na mashtaka yanayofaa yatafuata.

Video hiyo ilizua taharuki kwenye mitandao ya kijamii huku wengi wakitaka hatua zichukuliwe.

"Walichofanya kinaweza tu kuitwa tukio la kishenzi, kinyama, na kichaa. Haina uhalali wowote! Wacha wakabiliane vikali kisheria,” Mkenya mmoja kwenye Twitter alisema.

"Naunga mkono kukamatwa kwa walimu hao sita ... Hakuna uhalali wa walichokifanya," aliongeza.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post