Kesi Ya Cassie Yamuibua Ex Wa Diddy

Kesi Ya Cassie Yamuibua Ex Wa Diddy

Ikiwa ni wiki ya tano tangu kesi ya mkali wa Hip Hop, Marekani aianze kusikilizwa mashahidi wameendelea kutoa ushahidi wao ambapo siku ya jana Juni 9,2025 aliyekuwa mpenzi wa Diddy ambaye amefahamika kwa jina bandia la Jane aliendelea kutoa ushahidi ikiwa ni siku yake ya tatu kusimama kizimbani.

Jane aliiambia mahakama kuwa alipata mshituko mkubwa baada ya kuona kesi ya Cassie Ventura na kugundua madai mengi yaliyotolewa na Cassie yalikuwa yanafanana kabisa na ya kwake ambapo alichukua jukumu la kupiga picha skrini (screenshots) za kurasa tatu za kesi hiyo na kuzitunza.

Utaumbuka Ventura aliwasilisha kesi dhidi ya Diddy Novemba 2023, akimshutumu kwa makosa mbalimbali ya kingono, yakiwemo kumlazimisha kushiriki tendo la ngono na wanaume waliolipwa (male escorts), kumlazimisha kutumia dawa za kulevya haramu, kumbaka na kumpiga.

Aidha Jane alieeleza kuwa siku tatu baada ya Ventura kuwasilisha kesi hiyo, alipokea simu kutoka kwa Diddy mazungumzo ambayo yalisikilizwa mahakamani rekodi ambazo zilipatikana kutoka kwa mfanyakazi wa zamani wa Combs, Kristina Khorram. Ambapo Diddy alimwambia Jane kwamba matukio yote waliyofanya ni mambo ya kimapenzi ambayo waliyafurahia wote.

Hata hivyo, Jane alimjibu kuwa matukio yote hayakuwa vile ambavyo yeye anasema kisha akakata simu. Lakini alipokea simu nyingine ya vitisho kutoka kwa nyota huyo akimwambia kuwa atamtumia baba mtoto wake video za ngono ambazo alirekodiwa kwa hiyari yake.

Jane alipanda kizimbani kwa mara ya kwanza Juni 6, 2025, katika Mahakama ya Shirikisho ya Manhattan, ambapo alijitambulisha kama mpenzi wa zamani wa Diddy ambaye alikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na rapa huyo kuanzia mwaka 2021, hadi alipokamatwa mwaka 2024.

Alieleza kuwa Diddy alimlazimisha kushiriki kufanya matukio ya kingono yaliyojaa matumizi ya dawa za kulevya na wanaume waliolipwa, licha ya kufanya juhudi za kujiondoa kwenye matukio hayo Combs alimtishia kutomsaidia kifedha.

Sean "Diddy" Combs alikamatwa Septemba 16, 2024 katika Hoteli ya Park Hyatt, Manhattan, New York na kupelekwa moja kwa moja katika gereza la Metropolitan huko Brooklyn. Kesi yake ilianza kuzikilizwa Mei 5, 2025 huku mashahidi zaidi ya 15 wakitoa ushahidi akiwemo Kid Cudi, Mia, Cassie Ventura, mama mzazi wa Cassie, Bryana Bongolan na wengineo.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags