Abby alikuwa akiwania tuzo hiyo akishindanishwa na mastaa mbalimbali akiwemo Shallipopi, Merveille, Dlala Thukzin, Maglera Doe Boy, kwn, TxC, Odeal, Dr. Yaro, Amabbi na Ajuliacosta ambaye ameshinda tuzo hiyo.
Licha ya kuwepo kwa jitihada nyingi kutoka kwa Serikali na mastaa mbalimbali hapa nchini kumsapoti msanii huyo huku ikionekana kupata muitikio mkubwa kupitia Instagram ya BET, lakini mashabiki wanashangaa msanii huyo kuangukia pua kama wasanii wengine.

Watu walifeli hapa
Kushinda tuzo za BET, hasa kwenye kipengele cha Best New International Act, hakutegemei tu idadi ya likes au comments kwenye mitandao ya kijamii kama Instagram. Ingawa ushiriki wa mashabiki kwenye mitandao ni muhimu kwa kuonyesha sapoti, kura rasmi za ushindi hupigwa kupitia tovuti ya BET.
Kwa bahati mbaya, upande wa Bongo, mashabiki wengi walijikita zaidi kwenye kuonesha upendo katika mitandao ya kijamii, lakini hawakufuata hatua muhimu ya kupiga kura kwenye tovuti ya BET ambapo ndio hupelekea msanii kushinda.
Vigezo vya BET ili msanii aweze kunyakuwa Tuzo
Tuzo za BET huzingatia mambo mbalimbali katika kuamua washindi, ikiwa ni pamoja na mauzo, ubora wa jumla wa kazi zilizotolewa, athari ya kitamaduni, na umaarufu wa msanii kwa mashabiki hata hivyo baadhi ya vipengele huzingatia mambo mengine kama ubunifu, maono ya kisanii na mchango kwa jamii.
Kwa ujumla wagawaji wa tuzo hizo huangalia vitu mbalimbali kwa msanii ambavyo ni pamoja na mauzo na mafanikio ya kibiahsara, msanii hupimwa kwa kiasi cha mauzo ya muziki wake, mafanikio ya kimauzo kwenye majukwaa ya kidijitali, ubora wa kazi zake ukianziwa na ubunifu, uandishi wa nyimbo, uzalishaji wa muziki na ubora wa video.
Lakini pia msanii anaangaliwa kama ana ushawishi mkubwa kwa jamii hasa ndani ya tamaduni za watu weusi kwa kuangalia kazi zake kama zinazungumzia maisha, changamoto na mafanikio ya watu weusi, ambapo msanii akiendana na sifa hizi basi kuna nafasi kubwa ya kushinda tuzo hiyo.
Vilevile, kuangalia ushiriki na mashabiki wake ambapo msanii atatakiwa kuwashawishi mashabiki kumpigia kura (fan voting) ambapo wasanii wenye ushawishi mkubwa basi uwezo wao wa kushinda tuzo ni mkubwa, pia msanii awe na maono ya kisanii, rekodi ya mafanikio kwa mwaka na ushawishi wake wa Afrika na dunia nzima.
Hata hivyo, ukiachilia mbali mashabiki kupiga kura katika mitandao ya kijamii, lakini pia ili kujiweka katika nafasi ya kushinda mashabiki inabidi kukupigia kura kupitia tovuti rasmi ya BET hasa kipengele cha Best New International Act. Hata hivyo kwa mujibu wa tovuti mbalimbali baadhi ya vipengele kura hupigwa na jopo la BET.
Utakumbuka mwaka 2014 historia hiyo ilishikiliwa na mwanamuziki Diamond Platnumz akiiwakilisha Tanzania kwa mara ya kwanza katika kuwania kipengele hicho ambacho awali kilifahamika kama ‘Best International Act: Africa’.
Baada ya kugonga mwamba mwaka huo, Diamond alijaribu tena bahati yake mwaka 2016 na 2021 lakini hakufanikiwa kutwaa tuzo hiyo. Hata hivyo, mbali na Diamond, Rayvanny naye alitajwa kuwania tuzo hizo katika kipengele cha Viewer’s Choice na kufanikisha kushinda huku akiwa msanii pekee kutoka Bongo kushinda tuzo hizo za BET.
Leave a Reply