Rapa maarufu kutoka Marekani, Ricky Lamar Hawk 'Silentó' (27) amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kumuua binamu yake ‘Frederick Rooks III’ mwaka 2021.
Wakili wa kesi hiyo kutoka wilaya ya DeKalb, alitangaza Jumatano kwamba rapa huyo mwenye umri wa miaka 27, alikiri kosa la kuua bila kukusudia, kufanya shambulio la kikatili, kumiliki bunduki, na pia kuficha kifo cha binamu yake Frederick.
“Kama tulivyokuambia, baada ya muhalifu kufanya tukio hilo Polisi wa DeKalb walikuta mwili wa marehemu Rooks ukiwa na majeraha mengi ya risasi, huku eneo la tukio likitapakaa maganda ya risasi",”Alisema wakili
Hata hivyo, baada ya uchunguzi wa polisi kukamilika walibaini picha kwenye CCTV Camera zikimuonesha Silentó akikimbia eneo hilo la tukio kwa gari nyeupe aina ya BMW.
Pia uchunguzi wa Polisi hao ulihusisha upimaji wa Ballistic Testing ili kulinganisha maganda ya risasi yaliyopatikana katika eneo la tukio nakujiridhisha yaposawa na bunduki inayomilikiwa na Silentó.
Inaelezwa kuwa siku 10 baada ya tukio hilo, rapa Silentó alikiri kuhusika katika mauaji hayo lakini ulitokea mzozo mkubwa akijitetea kuwa na tatizo la afya ya akili alilokuwa nao tangu akiwa mtoto ambapo inasemekana alijaribu hata kujitoa uhai mwaka 2020.
Aidha hakimu wakesi hiyo bado aliona miaka 30 ilikuwa adhabu inayomfaa rapa huyo aliyejipatia umaarufu mkubwa baada ya kuchia wimbo wake wa 'Watch Me (Whip/Nae Nae)' mwaka 2015, ngoma ambayo imetazamwa zaidi ya mara bilioni 1.9 kwenye mtandao wa Youtube.

Leave a Reply