Filamu 68 zapenya ZIFF 2025, Kombolela, Jacobs Daughter zatajwa

Filamu 68 zapenya ZIFF 2025, Kombolela, Jacobs Daughter zatajwa

Filamu 68 zitachuana kuwania tuzo katika Tamasha la 28 la Kimataifa la Filamu (ZIFF) linalotarajiwa kuanza kufanyika Juni 25 hadi 29, 2025.

Filamu hizo zilizochaguliwa ni kati ya filamu 430 zilizowasilishwa kushiriki katika tamasha hilo ambalo hufayika kila mwaka.

Akizungumza na waandishi wa habari leo June 13, 2025 Mkurugenzi wa Tamasha hilo Hatibu Madudu amesema kwa mwaka huu wamepokea jumla ya filamu 430 idadi ambayo ni tofauti na mwaka jana ambapo walipokea zaidi ya filamu 3000.

"Mwaka huu tumepokea ambazo zimezalishwa mwaka 2024-2025 tu, tumekuwa na mshangao kwa kiwango kikubwa cha filamu ambacho tumekitapa kwa zilizotengenezwa ndani ya mwaka mmoja tu. Katika filamu hizo Afrika Mashariki ni filamu (174) ambazo Kenya (54), Uganda (52), Tanzania (49), Rwanda (6), Burundi (1), Congo (4), Somaria (8), "amesema

Amesema nchi nyingine ambazo zimeongoza kuwasilisha kazi kwa wingi mwaka huu ni Iran
(79), Afrika Kusini(20), Egypt (36) huku akisema yapo na mataifa mengine mengi zaidi ya 100 kama India, China, Ufaransa, Uturuki, Nigeria, Japan na nyinginezo.

"Filamu zimegawanyishwa katika makundi haya short films and animation 28, Tv drama series 10, Documentary film 14, feature fiction film 15 ndizo zinafanya kuwa na filamu 29 zilizochaguliwa ZIFF 2025, "anasema Madudu

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa ZIFF Joseph Mwale amesema kaulimbiu ya mwaka huu isemayo "Tumaini Linapochipukia" (Where hope takes root) inaonesha vitu ambavyo sinema zinaweza kufanya.

"Filamu siyo tu burudani lakini inabeba stori inatukumbusha hata kwenye giza tumaini linatafuta nafasi ya kukua. Kwa mwaka huu kila filamu utayoona ni mbegu zilizopandwa na watengenezaji filamu waliojaribu kuamini kwamba stori zinaweza kuchipusha mizizi kwenye mioyo, napenda kuwakaribisha wote kwenye hili tukio, "amesema Mwale

Kati ya kazi za wasanii nchini zilizoingia kwenye kinyang'anyiro ni Jenina ya Emmanuel Gembe, My Son ya Ramar King na Isarito Mwakalindile, Jacobs Daughter ya Leah Mwendamseke (Lamata), Jivu (Mustapha Machupa), Kombolela (Mustapha Machupa) na nyinginezo






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags