Dj Mushizo Apata Ajali Ya Moto, Meneja Asimulia

Dj Mushizo Apata Ajali Ya Moto, Meneja Asimulia

Meneja Msaidizi wa Dj Mushizo, Ally Masupu amesema chanzo cha moto kilichosababisha msanii huyo kupata ajali ya moto ni shoti ya umeme.

Mashizo alikumbwa na ajali hiyo jana saa 12 jioni, Juni 12,2025 wakati akiwa nyumbani kwake Tabata Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Mwananchi, Masupu ameeleza kuwa wakati wa moto Mushizo alikuwa amelala jambo ambalo lilisababisha wananchi kung'oa bati ili kumuokoa.

“Dj Mushizo anaendelea vizuri, matibabu yameanza jana mpaka leo, kiufupi anaendelea vizuri japokuwa amejeruhiwa sana na moto kama picha zinavyoonesha lakini kwa sasa Mwenyezi Mungu anabariki anaendelea vizuri.

"Chanzo cha moto ni shoti ya umeme pale ndani anapoishi Tabata, yeye alikuwa amelala hana habari, alipokuja kushtuka akakuta moto umeshashika kasi, hakuweza kujiokoa mwenyewe,” amesema Masupu.

Aidha ameendelea kwa kusema kuwa “Wananchi wakatoka wakachomoa bati kwa juu, wakaenda kumtoa ndani. Amelazwa katika Hospitali ya Amana kwa ajili ya matibabu zaidi japokuwa huduma ya kwanza alipatiwa Tabata. Wakati moto unaendelea alikuwa mwenyewe ndani, ingawa siku zote anakuwaga na kijana wake anayekaa naye nyumbani lakini jana alikuwa ametoka kidogo kwa hiyo akawa amebaki mwenyewe,” amesema Masupu.

Taarifa za kupata kwa ajali hiyo zilichapishwa katika mitandao ya kijamii ya Mushizo ambapo ilieleza.

“Nimepata ajali ya moto jioni ya leo baada ya ninapoishi kushika moto na mimi nilikuwa nani ya nyumba namshkuru Mungu nipo hospitali now naendelea na matibabu, maombi yenu ndugu zangu sana.”

Nyimbo zilizompa Mashizo umaarufu unajulikana kwa jina la Wivu pamoja na Mapenzi Hisia, ambazo zinafanya vizuri kwa sasa.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags