Miaka 25 ya Westlife waja kivingine, mmoja ajitoa

Miaka 25 ya Westlife waja kivingine, mmoja ajitoa

Kundi la muziki kutoka Ireland, ‘Westlife’ ambalo lilitamba na ngoma zake kama ‘My Love’, ‘Soledad’ katika miaka ya 2000, limeripoti kutimiza miaka 25 huku likiwa na mpango kabambe wa kutoa burudani kwa kufanya ziara katika kusherehekea miaka hiyo.

Kupitia ukurasa wao wa Instagram, kundi hilo limethibitisha kuandaa tamasha kusherehekea maadhimisho ya miaka 25 huku likiweka wazi kuwa mwanakikundi mwenzao, Mark Feehily hatakuwa sehemu ya maadhimisho hayo.

“Tuna furaha kubwa kutangaza uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 25, Februari 9, 2001 tulianza ziara yetu ya kwanza kabisa duniani katika Ukumbi wa Newcastle Arena. Nani angefikiri kwamba bado tungekuwepo hapa miaka 25 baadaye? Tuna mipango mingi ya kusisimua tutakayoshiriki nanyi hivi karibuni, ikijumuisha muziki mpya, albamu, maonyesho maalum, na mshangao mwingi zaidi njiani.

Kwa masikitiko, Mark hataweza kushiriki kwenye maadhimisho haya. Tunatumaini ataweza kujiunga nasi jukwaani pindi atakapokuwa tayari na mwenye uwezo. Kama kawaida, anawatakia nyote kila la kheri. Sisi wanne hatuamini bado kuwa ni miaka 25 imepita.

Tulikuwa tunaota tu kuhusu upendo na uaminifu wa kudumu mnaoendelea kutuonyesha kutoka kote duniani. Tuna bahati sana kuwa na ninyi wote pamoja nasi na hatuwezi kusubiri kusherehekea pamoja. Heri ya Miaka 25 Kwetu Sote,” imeeleza taarifa hiyo.

Hii sio mara ya kwanza kwa Mark kujiondoa kwenye makundi, inaelezwa kuwa mwaka 2024 alijiondoa katika kundi lililoundwa na Shane Filan, Kian Egan na Nicky Byrne kutokana na matatizo ya kiafya.

Kundi la Westlife lilianzishwa mwaka 1998 na Louis Walsh likijumuisha wasanii watano ambao ni Shane Filan, Mark Feehily, Kian Egan, Nicky Byrne na Brian McFadden ambaye alijiondoka mwaka 2004 katika kundi hilo.

Westlife walijulikana kufuatia na nyimbo zao za mapenzi na sauti ya kuvutia ambapo walipata umaarufu miaka ya 2000 huku wakiuza rekodi ya nyimbo zao zaidi ya milioni 55 duniani kote, huku nyimbo zao 14 zikiongoza kwenye chati za Uingereza ikiwemo "Flying Without Wings", "Swear It Again", "Uptown Girl", "You Raise Me Up", "World of Our Own" na nyinginezo.

Hata hivyo kundi hilo lilitangaza kusitisha shughuli zake za muziki mwaka 2012 lakini lilirudi tena mwaka 2018 na kuendelea kutoa muziki pamoja na kufanya maonesho katika nchi mbwalimbali.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags