Kanye West Abadili Jina Tena, Sasa Anaitwa YE YE

Kanye West Abadili Jina Tena, Sasa Anaitwa YE YE

Rapa na mjasiriamali wa mitindo, Kanye West, ambaye anafahamika pia kama 'Ye' amebadilisha tena jina lake na sasa anatambulika kama 'Ye Ye' ikiwa ni miaka minne tangu alipoachana rasmi na jina lake la awali, Kanye West, na kujulikana kisheria kama Ye.

Kwa mujibu wa nyaraka zake mpya za kibiashara zilizopatikana huko California, msanii huyo sasa anajiita Ye Ye. Taarifa hizi zimethibitishwa na gazeti la Page Six, likimkuu afisa wake mkuu wa fedha, Hussain Lalani ambaye aliwasilisha nyaraka rasmi za kuthibitisha mabadiliko hayo.

Jina hilo la Ye Ye, tayari limeanza kutumika katika baadhi ya kampuni zake maarufu, zikiwemo Yeezy Apparel, Yeezy Record Label LLC, na Getting Out Our Dreams Inc.

Hapo awali, West alishawahi kutumia jina la Ye West katika baadhi ya usajili wake wa kibiashara.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Masoud Kofii


Latest Post

Latest Tags