Mondi, Blue, Jay Melody wagusa hisia za Tale

Mondi, Blue, Jay Melody wagusa hisia za Tale

Diamond, Mr Blue na Jay Melody wamkosha Babu Tale kwenye wimbo wao mpya uitwao 'Mapozi' uliachiwa saa kumi zilizopita.

Kupitia post ya Diamond kwenye mtandao wa Instagram ambayo ameweka kipande cha wimbo huo mpya, Tale ameshindwa kuzuia hisia zake na kudondosha comment isomekayo,

"Muunganiko wa vijana kutoka mkoa wa Morogoro umenikosha sana hapa @diamondplatnumz kule @realjaymelody mix mzaramo wa dar @mrbluebyser1988".

Tale ni Meneja wa Diamond na Mbunge wa Morogoro Kusini Babu Tale. Hadi sasa wimbo huo unawatazamaji 237k kwenye mtandao wa YouTube.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post