Ikulu ya Marekani imezindua akaunti rasmi kwenye TikTok inayomilikiwa na Wachina ikiwa bado mwezi mmoja kuanza utekelezaji wa ahizo la Rais Trump kupiga marufuku jukwaa hilo la mitandao ya kijamii kutumika nchini Marekani.
Sheria ya Ulinzi wa Data ya Mwaka 2024 ilitaka TikTok kusitisha shughuli zake ifikapo Januari 19 mwaka huu isipokuwa kama ByteDance, ambayo ni kampuni mama ya programu hiyo iwapo ingepata leseni ya uendeshaji shughuli zake Marekani.
Trump, ambaye alikuwa mtumiaji mkubwa wa TikTok wakati wa kampeni zake za urais, aliongeza muda wa mwisho hadi mapema Aprili, kisha Juni 19 na kuwapa muda hadi Septemba 17.
Akaunti hiyo ya @WhiteHouse tayari imepata zaidi ya wafuasi 80,000 tangu izinduliwe jana Jumanne Agosti 19, 2025 kupitia video fupi iliyomwonyesha Rais na maandishi yaliyosomeka: “America we are Back! What’s up TikTok?”
Awali, Rais Trump alitahadharisha kuwa kutumia TikTok nchini humo kuwa ni hatari kwao. Kauli hiyo aliitoa aliposaini agizo la kiutendaji mwaka 2020 lililoweka vikwazo vingi dhidi ya programu hiyo wakati wa muhula wake wa kwanza wa urais.

Leave a Reply