Nandy Athibitisha Kupokea Sh100 Milion Kutoka Kwa Yammi

Nandy Athibitisha Kupokea Sh100 Milion Kutoka Kwa Yammi

Mwanamuziki na mmiliki wa Lebo ya ‘The African Princess’ Nandy amethibitisha kupokea kiasi cha Sh100 milioni kutoka kwa aliyekuwa msanii wake Yammi kama asante na kuondoka katika lebo hiyo.

Nandy ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuulizwa kiasi alichopokea kutoka kwa msanii huyo ambapo ameeleza kuwa licha ya Yammi kutoa kiasi hicho lakini Lebo yake ilihitaji zaidi ya pesa hizo.

“Ni kweli alilipa pesa hizo, na ndivyo mkataba ulivyo ukiwa unataka kutoka kabla ya mkataba kukamilika kunagharama ambazo unatakiwa na nafikiri haikuwa bei hiyo ilikuwa zaidi ya hiyo lakini kutokana na mahusiano yetu mazuri, bado ni mtoto mdogo anajitafuta tulimpa nafasi ya yeye kuamua anataka kulipa bei gani, theni akawa tayari kulipa kiasi hicho tukapokea kama asante,”amesema Nandy.

Akieleza kuhusu kutokupokea simu ya Yammi, Nandy ameeleza kuwa msanii huyo anayetamba na ngoma ya ‘Raha’ hajawahi kumpigia simu.

“Kiukweli hakunipigia hata mimi mwenyewe nilimtafuta Dm sehemu ambayo anapenda kuingia sana, nikamtumia ile interview ambayo niliiona nikamuuliza ulinipigia simu lini sikupokea. Lakini yeye alichonijibu aliibiwa simu na hakuwa na namba so basi akaomba msamaha ikaishia hivyo,”amesema Nandy.

Ikumbukwe wakati wa uzinduzi wa wimbo wake wa ‘Raha’ uliofanyika Juni 5,2025 mwanamuziki Yammi aliweka wazi kiasi alicholipa ili kuondoka katika lebo hiyo huku akidai kuwa Nandy alihitaji pesa nyingi zaidi.

“Sijalipiwa na lebo yoyote wala menejimenti, kwenye maisha hapa kuna watu wengi wana roho nzuri sana wasamaria wema, kila mtu ana msaidizi wake, ni mtu tuu aliona mimi ni mtoto mzuri nina tabia nzuri, namfurahisha mpole akaamua anisaidie.

"Alilipia Sh100 milioni, ilikuwa ni zaidi ya hapo lakini baada ya kuongea naye kama dada akapunguza,”amesema Yammi.

Lebo ya Nandy ilitangaza kutemana na msanii huyo mwezi Mei mwaka huu, ambapo aliingia katika lebo hiyo Januari 20, 2023.

Yammi alisaini mkataba na The African Princess baada ya Nandy kuvutiwa na video zake za uimbaji kwenye TikTok. Baada ya kusainiwa, alitoa EP yake ya kwanza yenye nyimbo tatu ambazo ni Namchukia, Tunapendezana, na Hanipendi, ambazo zilipokelewa vyema na mashabiki.

Katika kipindi chote akiwa chini ya lebo hiyo, Yammi alifanikiwa kujizolea umaarufu mkubwa, akiwa miongoni mwa wasanii wa kike waliopata streams nyingi zaidi kwenye Boomplay mwaka 2023, huku akitanguliwa na Zuchu na Nandy.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post

Latest Tags