Mawakili wa Iran wawakosoa hadharani viongozi wa kidini

Mawakili wa Iran wawakosoa hadharani viongozi wa kidini

Mawakili arobaini mashuhuri Iran, wanaotetea haki za binaadamu wamewakosoa hadharani viongozi wa kidini, wakisema utawala uliopo utaondolewa madarakani, kufuatia waandamanaji kote nchini humo kutoogopa tena kamata kamata inayofanywa na serikali dhidi yao.

Mawakili hao ambao baadhi ni wa kutoka ndani ya nchi na wengine nje ya nchi, wamesema serikali inaendelea kuota ikiamini inaweza kukandamiza, kukamata na kuua kwa lengo la kunyamazisha.

Maandamano nchini humo yamechochewa na kifo cha msichana wa miaka 22 Mahsa Amini kilichotokea wakati alipokamatwa na polisi wa maadili, kufuatia kutovalia vizuri hijabu yake.

Maandamano hayo yameliyumbisha tabaka la mashehe, huku kiongozi Mkuu Iran Ayatollah Ali Khamenei na rais wa taifa hilo Ibrahim Raisi wakiwa viongozi wa kidini, na watu wa matabaka mbalimbali nchini humo wakidai mabadiliko ya kisiasa katika Jamhuri hiyo ya kiislamu.

 






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post