Ingawa hakufanikiwa kutwaa tuzo hiyo, heshima ya kutajwa pamoja na mastaa wakubwa ilikuwa ushindi kwa tasnia ya muziki wa Tanzania. Ushindi ulienda kwa msanii kutoka Brazil, Ajuliacosta, ambaye alikonga nyoyo za mashabiki kwa shukrani za dhati na ujumbe wa matumaini kwa wasanii wapya duniani.

Usiku huo pia ulimvusha msanii wa Hiphop nyota tokea Marekani, Kendrick Lamar ambaye ameibuka kinara kwa ushindi wa tuzo nyingi zaidi. baada ya kutwaa tuzo tano ambazo ni Album Bora ya Mwaka (GNX), Msanii Bora wa Hip Hop, Video Bora ya Mwaka kupitia kazi yake “Not Like Us.”, Wimbo Bora wa Kushirikiana 'Luther' akiwa na mwanadada SZA, Lamar pia ameshinda tuzo ya muongozaji bora wa video wa mwaka na mshirika wake wa muda mrefu katika ubunifu 'Dave Free'. Utakumbuka kuwa rapa huyo pia aliibuka kinara kwenye tuzo za Grammy 2025 baada ya kushinda vingele vitano.
Kwa upande wa wanawake, Doechii ameibuka kidedea kama Msanii Bora wa Kike wa Hip Hop, akitumia jukwaa hilo kulaani ukandamizaji wa haki za raia na mashambulizi dhidi ya wahamiaji. Wakati huo huo, SZA alizawadiwa kama Msanii Bora wa R&B/Pop wa Kike, akionekana kugusa hisia za wengi kwa uimbaji wake wa kipekee, huku tuzo ya Msanii Bora wa R&B/ Pop wa Kiume ikienda kwa Chris Brown.
Washindi wengine ni pamoja na Leon Thomas ambaye ameshinda Msanii Bora Chipukizi, Denzel Washington Mwigizaji Bora wa Kiume na Cynthia Erivo Mwigizaji Bora wa Kike, Ang'el Reese ambaye ameshinda Mwanamichezo Bora wa Kike, Jalen Hurts Mwanamichezo Bora wa Kiume, Blue Ivy Carter ameshinda tuzo ya Youngstar, Luther: Never Too Much Imeshinda kama Movie Bora.
Mariah Carey, Jamie Foxx, Kirk Franklin na Snoop Dogg pia walikuwa miongoni mwa waliotunukiwa tuzo ya Heshima ya 'Ultimate Icon ya 2025'.
Ulipofika wakati wa Jamie Foxx, aliyepewa tuzo ya heshima yani 'Ultimate Icon Honor' kwa mchango wake mkubwa kwenye muziki na filamu. Machozi yalimtoka aliposhukuru kwa nafasi ya pili ya kuishi baada ya kuumwa kwa muda mrefu akisema: “Wakati huu siwezi kuipoteza tena.”
Usiku huo msanii aliyekuwa akiwania Tuzo nyingi zaidi ni rapa Kendrick Lamar ambaye aliongoza baada ya kuteuliwa katika vipengele kumi, akifuatiwa na Doechii, Drake, Future na GloRilla ambao walikuwa wakiwania vingele sita kila mmoja, Metro Boomin alikuwa anawania vipengele vitano, huku SZA na The Weeknd walikuwa wakiwania vipengele vinne kila moja.

Wakati wa hafla hiyo wasanii waliyopewa jukumu la kutumbuiza kwenye jukwaa hilo ni pamoja na GloRilla, Ledisi, Leon Thomas, Lil Wayne, Playboi Carti na Teyana Taylor walikuwa miongoni mwa waliopanda jukwaani kutumbuiza.
Usiku wa hafla hiyo ya Tuzo za BET zilizokuwa zinafanyika kwa mara ya 25 tangu kuanzishwa kwake, zilikuwa zikiongozwa 'Hosted' na mchekeshaji, Kevin Hart katika ukumbi wa Peacock huko Los Angeles.
Leave a Reply