Watu wachangamkiza nguo za Kim Kardashian

Watu wachangamkiza nguo za Kim Kardashian

Waswahili wanasema ‘namba’ hazidanganyi na hii imejidhihirishia siku ya jana Alhamisi 26, 2023 katika uzinduzi wa nguo za kiume kutoka kwenye chapa ya SKIMS MENS inayomilikiwa na mfanyabiashara Kim Kardashian kwa kukusanya mamilioni ya ‘dola’ ndani ya dakika. 

Vyanzo vya karibu vya mfanyabiashara huyo vinaeleza kuwa SKIMS MENS ilivunja ‘rekodi’ baada ya zaidi ya watu 20,000 ndani ya dakika tano kuagiza nguo hizo na kufanya chapa hiyo kuingiza mamilion ya ‘dola’ kwa dakika.

Nguo hizo za kiume zilifanyiwa ‘promo’ na mchezaji kutoka ‘klabu’ ya Al Hilal ya Saudi Arabia, Neymar akiwa na Nick Bosa na Shai Gilgeous-Alexander.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post