Perry afariki kwa mshutuko

Perry afariki kwa mshutuko

Muigizaji kutoka nchini Marekani Matthew Perry amefariki dunia baada ya kupata mshtuko na kudondokea kwenye Jacuzzi nyumbani kwake Los Angeles jana Jumamosi.

kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo vinaeleza kuwa msanii huyo kabla ya kifo chake alikuwa akicheza mchezo wa #Pickleball, nyumbani kwake, ghafla akapata mshtuko na kudondokea kwenye Jacuzzi.

Mpaka sasa hakijajulikana chanzo rasmi cha kifo chake ingawa maofisa wa polisi nchini humo wanaendelea na uchunguzi juu ya kifo cha msanii huyo.

Ikumbukwe kuwa msanii huyo mwenye umri wa miaka 54 aliwahi kupata umaarufu katika filamu mbalimbali ikiwemo ya Chandler Bing, Sunshine.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post