Messi alivyopokelea Inter Miami

Messi alivyopokelea Inter Miami

Kama ilivyo kawaida kwa wachezaji wakubwa katika nchini mbalimbali kupeleka tuzo walizoshinda katika ‘timu’ wanazo zichezea, Lionel Messi naye amefanya hivyo baada ya kushinda Tuzo ya Bollon d’or 2023 amerudi na kutua nayo katika ‘timu’ ya vijana katika ‘Klabu’ ya Inter Miami.

Kupitia ukurasa wa Instagram ya Inter Miami wame-share video ikimuonesha Messi akiwa amebabe sanduku lililokuwa na tuzo yake ya nane na kwenda nayo katika uwanja wa mazoezi wa ‘timu’ ya vijana na kupiga nao picha.

Kuoitia post hiyo Inter Miami wameandika kuwa wamefanya hivyo kwa ajili ya kuwa-inspire wachezaji wenye ndoto kama za mchezaji huyo.

Ikumbukwe Lionel Messi amenyakua Tuzo hizo mwaka 2009, 2010, 2011, 2012, 2015, 2019, 2021 na 2023.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post