Moja ya tukio ambalo limepokea maoni mengi kutoka kwa mashabiki na mastaa katika shamra shamra za ugawaji wa tuzo za Trace ni kuhusiana na mwanamuziki Diamond kusafirisha gari (ndinga) zake kutoka Dar hadi Zanzibar.
Kutokana na tukio hilo kupata maoni mbalimbali wakati alipokuwa kwenye mahojiano kwenye ‘Blue Carpet’ kwenye usiku wa Trace Awards, Diamond aliweka wazi sababu ya kufanya hivyo ni kwa ajili ya kuiheshimisha nchi.
“Unajua hii sehemu watu wanatazama so lazima ufanye uwekezaji kwahiyo nikaona nikifanya hivi na watu wakiona inaweza kuleta heshima kwa nchi, taifa na kwenye muziki wetu
Mimi kinapotokea kitu napenda kufanya kitu tofauti, nikajiuliza nifanye kitu gani so nikaona miongoni wa utofauti wacha nipeleke magari kwa sababu sio kila mtu anaweza kufanya na watu sio kama hawawezi kufanya wanaweza lakini mimi nikaona wacha nifanye kitu kipya, nimeamua kufanya hivyo na nimeshukuru watu wamelipokea kwa ukubwa kama nilivyotaka,”amesema Dimaond
Utakumbuka ambaye anatambulika kimataifa kupitia ngoma ya ‘Komasava’ alisafirisha ndinga zake tatu ambazo ni Simba, Simba 1 na Simba 2 ambayo haiingi risasi.

Leave a Reply