Kwa mara ya kwanza mwingizaji na mfanyabiashara Jacqueline Wolper amezungumza kuhusiana na kesi inayomkabili mwigizaji mwenzie Joice Mbaga 'Nicole' ambaye alifunguliwa kesi ya uhujumu uchumi kwa kupokea amana (fedha) kutoka kwa umma bila kibali cha Benki Kuu (BoT).
Wolper ameweka wazi kuwa hajawahi kusikia ‘skendo’ yoyote ya msanii huyo ya kuwa mwizi, huku akidai Sh 180 milioni kwa Nicole ni pesa ndogo.
“Sh 180 milioni ni hela ndogo sana na kwa msanii kama Nicole ninavyomjua mimi ni hela ndogo sana. Sidhani kama fedha ndogo kama ile inaweza kumchafua, unajua sisi binadamu kuna vitu vingi sana lakini pia tunapitia vitu vingi sana. Kuna watu wananguvu zao na uwezo wa kufanya wanavyojua wenyewe.
"Kwa hilo siwezi kuliongelea na siwezi kulizungumzia lakini naweza kusema. Sidhani kama ni hela ambayo inaweza kumshinda Nicole kwa sababu kama yeye ni mpambanaji, nadhani mnamuona anavyopambana kila siku. Anavyopiga domo, anatangaza hadi matangazo ambayo hayafai kwahiyo ni mtafutaji ni mpambanaji,”amesema Wolper
Ikumbukwe Nicole alikaa rumande kwa siku 15 na mwenzake Rehema Mahanyu (31), wanaokabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi, waliachiwa Machi 17, 2025, kwa dhamana ya nyumba.
Aidha baada ya kupandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kivukoni inayoketi Kinondoni, Jumatatu Machi 10, 2025, wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ambayo ni kupokea amana (fedha) kutoka kwa umma bila kibali cha Benki Kuu (BoT).

Leave a Reply