Mfanyabiashara Zari The Boss Lady ambaye pia ni mzazi mwenza wa msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ametia neno kufuatia ndoa ya Zuchu na Simba huku akiwapongeza kwa hatua hiyo.
“Kama ni kweli, nawatakia kila la heri lakini mimi na Mondi jinsi tulivyokuwa sasa tunashirikiana vizuri kwenye malezi ya watoto pamoja, watoto wetu hakuna kitu wanakosa, baba T ni aina ya mtu ukimpigia simu watoto wanahitaji vitu fulani anafanya Alhamdulillah,” amesema Zari.
Pia, amemsifu mwanamuziki Zuchu kwakuwa na moyo wa uvumilivu muda wote kwani wanawake wengi wameshindwa kumvumilia Simba ikiwa ni pamoja na yeye.
“Zuchu ndio mshindi wa tuzo ya Mchumba Bora wa Mwaka, huo uvumilivu mimi kama Zari sina, ana nguvu sana mwanamke yule, watu wakimuangalia wanaweza wasione lakini sisi wote hatukuweza kufanya vile.
"Tanasha amekuja pale lakini alifeli, muangalie Zuchu amefanikiwa kusimama kwa hiyo nampongeza sana, natumaini Naseeb anaishinae vizuri sasa kwa sababu ni mke wake sasa sio mchumba na nimsanii wake inabidi abadilike kidogo, mimi ni mama na natumaini hata Naseeb kama baba hatamani kuyaona mabaya yanatokea kwa bintiye Tiffah,”amesema Zari.
Mbali na hayo, lakini pia ameeleza kuwa endapo wawili hao watafanya sherehe kubwa na kumpa mualiko basi atahudhuria katika sherehe hiyo pamoja na watoto wake.
“Bila shaka tutakuja na watoto kwa sababu mimi na Naseeb ni familia sasa yale ya zamani yameisha sasa tupo karibu, Sisi tupo karibu kama marafiki na wazazi zaidi ya tulivyokuwa wapenzi kwa hiyo tutakuja na itakuwa vizuri," amesema Zari.
Aidha, Zari amewapongeza Jux na mke wake Priscilla kwa kufunga ndoa huku akiwasifia wawili hao kuwa wanaendana.
“Hongera kwake ukiwaangalia ni wapenzi wanaopendana, wanaelewana na wanamuunganiko mzuri, watu wengi wanaolewaga kwa mataminio lakini hawana muunganiko, ukimuangalia Jux na Priscilla wanaendana" amesema Zari.
Diamond na Zari walianza mahusiano mwishoni mwa 2014, baada ya kukutana kwenye ndege. Kufikia 2015, wawili hao walibarikiwa mtoto wao wa kwanza wa kike Tiffah, lakini pia walipata mtoto mwingine wa kiume Prince Nillan mwaka 2016. Uhusiano wa ulivunjika mwaka 2018 huku wakibakia na ushirikiano mzuri wa kulea watoto wao wawili pamoja.
Kwa mujibu wa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Kawambwa alieleza kuwa amewafungisha ndoa Diamond na Zuchu miezi mitano iliyopita.
“Kwanini watu wanapenda watu wengine wazini, Diamondi na Zuchu ni kweli nimewafungisha ndoa mimi toka miezi mitano iliyopita, ila hilo swali lako unaloniuliza kuhusu wameachana mimi silifahamu, sababu kama wangekuwa wameachana Diamondi angekuja kuniambia mimi,”amesema Warid.

Leave a Reply