Wajawazito wanaokunywa pombe kushitakiwa

Wajawazito wanaokunywa pombe kushitakiwa

Akizungumza katika kongamano la kukuza uelewa kuhusu athari za unywaji pombe kwa wajawazito nchini Afrika Kusini, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Hendrietta Bogopane-Zulu amesema unywaji wa pombe husababisha madhara kwenye ubongo wa watoto.

Hivyo amesema akinamama wanaokunywa pombe wakati wa ujauzito nchini humo washitakiwe maana ni unyayasaji wa watoto.

Kwa mujibu wa takwimu, matumizi ya pombe nchini humo imeripotiwa kufikia 41.5% kwa wanaume na 17.1% kwa wanawake, wakazi wa mijini ni 33.4% na wa vijijini 18.3% hali hiyo imeonekana kuwa tishio kwa taifa hilo watu kuzidi kuathirika na ulevi wa pombe.

Aidha Hendrietta ameeleza Shirika la Afya Duniani #WHO limeitaja Afrika Kusini kuwa na kiwango cha juu zaidi cha walevi wa pombe duniani.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post